Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo akikata keki kuashiria upendo na umoja kwa wanawake wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kushiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kitaifa yalifanyika tarehe 8 Machi, 2025 Jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akisalimiana na Mkuu wa Hifadhi ya Mikumi Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi TANAPA, Augustino Masesa mara baada ya kutembelea hifadhi ya Mikumi.
Picha ya pamoja ikijumuisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu, Mkuu wa Hifadhi ya Mikumi Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi TANAPA, Augustino Masesa wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kutembelea hifadhi ya Mikumi
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akipokea zawadi ya tuzo kutoka kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo ambayo imeandaliwa na wanawake wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika taasisi.
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wanawake kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma mara baada ya kushiriki kwenye Kongamano la Kanda ya Kati lililofanyika tarehe 3 Machi, 2025 Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Mwongozo wa Upelelezi na Uendeshaji wa Mashauri ya Makosa ya Kimtandao uliofanyika Jijini Dodoma tarehe 13 Februari, 2025.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi azindua Mwongozo wa Upelelezi na Uendeshaji wa Mashauri ya Makosa ya Kimtandao tarehe 13 Februari, 2025 katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Viungo wa Idara ya Utenganishaji wa Shughuli za Mashtaka na Upelelezi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka walioshiriki kwenye mafunzo ya idara hiyo yaliyofanyika Makao Makuu Jijini Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi mbalimbali walioshiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Sheria Jijini Dodoma tarehe 3 Februari, 2025
Picha ya pamoja ikijumuisha Kaimu Mkurugenzi Divisheni ya Makosa ya Udanganyifu na Utakatishaji Fedha Bw. Christopher Msigwa akiwa na washiriki wa Kikao kazi cha Maafisa Viunganishi wa Sehemu ya Makosa ya Mazingira na Maliasili kinachofanyika kuanzia tarehe 28 hadi 30 Novemba, 2024 mkoani Morogoro.