Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

NATIONAL PROSECUTIONS SERVICES

Kitengo cha Huduma za Utafiti na Maktaba

Lengo: kutoa utaalamu na huduma katika utafiti wa kisheria, huduma za uchapishaji na maktaba.

Majukumu:

Kitengo hiki kitakuwa na majukumu yafuatayo:

(i) Kufanya utafiti wa kisheria katika uendeshaji wa mashtaka na masuala yanayohusiana nayo;

(ii) Kuwajulisha watumiaji wa maktaba kuhusu bidhaa mpya za sheria;

(iii) Kuwekea maktaba vifaa vya kutosha vya utafiti, nyenzo na nyaraka za rejea;

(iv) Kuweka katika maktaba katiba, sheria na nyaraka mbali mbali za kisheria;

(v) Kutunza vitabu vya rejea vya kesi, machapisho na majarida ya kisheria na magazeti;

(vi) Kutunza rejesta ya machapisho ya rejea;

(vii) Kuwezesha uazimaji wa machapisho ya rejea;

(viii) Kuanzisha mfumo wa ubadilishanaji wa sheria zinazohusiana na uendeshaji wa mashtaka na kazi kutoka nchi zilizo katika jumuiya ya madola na zisizo za jumuiya; na

(ix) Kushauri juu ya ununuzi wa machapisho ya kisheria.

Kitengo hiki kitaongozwa na Afisa Mkuu wa Maktaba.