Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

NATIONAL PROSECUTIONS SERVICES

Kitengo cha TEHAMA

Lengo: kutoa utaalamu na huduma kwa matumizi ya TEHAMA ;

Kitengo hiki kitakuwa na majukumu yafuatayo:

(i) Kutekeleza mpango mkakati wa TEHAMA na Serikali Mtandao;

(ii) Kuendeleza na kuratibu mifumo TEHAMA kwa kushirikiana na wakala ya serikali mtandao;.

(iii) Kuhakikisha kwamba vifaa na programu za TEHAMA zinasimamiwa na kutunzwa

(iv) Kuratibu na kutoa msaada katika ununuzi wa programu na vifaa vya TEHAMA;

(v) Kuanzisha na kuratibu matumizi ya mawasiliano ya barua pepe na mitandao;

(vi) Kufuatilia na kusimamia usalama wa mifumo ya mawasiliano na taarifa; na

(vii) Kufanya tafiti na kushauri juu ya matumizi ya tehama kama chombo cha kuboresha utoaji wa huduma.

Kitengo hiki kitaongozwa na Afisa TEHAMA Mkuu.