Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

NATIONAL PROSECUTIONS SERVICES

Kitengo cha Uhasibu na Fedha

Lengo: kutoa huduma za usimamizi wa kifedha na utunzaji wa vitabu vya vitabu vya kihasibu.

Kitengo hiki kitakuwa na majukumu yafuatayo:

Mishahara

(i)Kuandaa malipo ya mishahara ikiwemo makato yaliyoainishwa kisheria;

(ii)Usimamizi wa mishahara;

(iii)Kuandaa taarifaza pensheni; na

(iv)Kutunza kumbukumbu.

Ofisi ya Fedha

(i)Kuwasilisha orodha ya malipo hazina;

(ii)Kuweka fedha na kuwasilisha hundi benki;

(iii)Kuandaa ripoti ya kila mwezi;

(iv)Kulipa fedha/hundi kwa wafanyakazi na wateja (watoa huduma);

(v)Kulipa malipo ya jumla;

(vi)Kutunza vitabu vya fedha;

(vii)Kurekodi na kuhakiki masurufu yaliyotolewa; na

(viii)Kuandaa na kufanya malipo.

Mapato

(i)Kusimamia mapato kulingana na kanuni na miongozo;

(ii)Kukusanya kodi ya kila mwaka,ada za maombi na vyanzo vingine;

(iii)Kusimamia na kukusanya mapato; na

(iv)Usuluhishi wa kibenki.

Pensheni

(i)Kuandaa nyarakaza pensheni; na

(ii)Kutunza kumbukumbu za pensheni.

Bajeti

(i)Usimamizi wa bajeti;

(ii)Kufuatilia ugawaji na matumizi ya fedha;

(iii)Kuandaa taarifa za mwisho na taarifa nyingine za kifedha.

Uhakiki na ukaguzi wa awali

(i) Kuhakiki na kupitisha nyaraka za malipo kwa mujibu wa kanuni;

(ii) Kuhakiki nyaraka za kifedha kwa mujibu sheria, kanuni na miongozo

inayosimamia fedha za umma; na

(iii)Kutoa majibu kwa hoja za ukaguzi

Kitengo kitaongozwa na Mhasibu Mkuu.