Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

NATIONAL PROSECUTIONS SERVICES

Kitengo cha Ununuzi na Ugavi

Lengo: kutoa utaalamu na huduma za ununuzi na ugavi.

Kitengo hiki kitakuwa na majukumu yafuatayo:

(i) Kushauri juu ya ununuzi , usimamizi wa vifaa na usambazaji wake;

(ii) Kufuatilia na kuhakikisha michakato ya ununuzi na taratibu zake zinafuatwa kwa mujibu wa sheria ya ununuzi wa umma;

(iii) Kuandaa mpango wa ununuzi wa mwaka;

(iv) Kununua, kutunza na kusimamia ugavi kulingana mahitaji;

(v) Kutunza na kusimamia usambazaji wa vifaa vya ofisi;

(vi) Kutunza na kuhuisha kumbukumbu za ununuzi na ugavi;

(vii) Kutoa huduma za sekretarieti kwa bodi ya zabuni;

(viii) Kuweka vigezo / viwango na kufuatilia uhalisia wa thamani ya bidhaa na huduma zinazonunuliwa; na

(ix) Kuandaaa mpango kazi , taarifa ya utekelezaji na bajeti ya ununuzi ya kitengo

Kitengo kitaongozwa na Mkurugenzi.