Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

NATIONAL PROSECUTIONS SERVICES

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Lengo: kutoa utaalamu na huduma za habari, mawasiliano , mazungumzo na umma pamoja na vyombo vya habari.

Kitengo hiki kitakuwa na majukumu yafuatayo:

(i) Kupata na kusambaza taarifa kwaajili ya kuhabarisha umma juu ya sera, programu kazi na maboresho yanayofanyika;

(ii) Kuratibu utoaji wa taarifa kwenye vyombo habari;

(iii) Kufanya mazungumzo na umma pamoja na vyombo vya habari juu ya masuala yanayohusu ofisi;

(iv) Kuratibu maandalizi ya nyaraka za kisekta;

(v) Kuratibu maandalizi na uzalishaji wa makala za ofisi katika magazeti na majarida; na

(vi) Kuhuisha taarifa za kisekta kwenye tovuti.

Kitengo hiki kitaongozwa na Afisa Habari Mkuu.