Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

NATIONAL PROSECUTIONS SERVICES

Divisheni ya Mipango

Lengo:kutoa utaalamu katika maeneo ya mipango, utekelezaji wa bajeti, ufuatiliaji na tathmini.

Majukumu

Divisheni hii itakuwa na majukumu yafuatayo:

(i) Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa mipango na bajeti;

(ii) Kuratibu maandalizi ya michango kwenye hotuba ya bajeti ya waziri na ripoti ya kila mwaka ya uchumi;

(iii) Kuratibu maandalizi, utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini ya mipango ya maendeleo;

(iv) Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa miradi programu za maendeleo na ukusanyaji wa rasimali zinazohitajika;

(v) Kuandaa, kutekeleza na kuboresha mpango wa usimamizi wa vihatarishi;

(vi) Kuandaa rejesta ya vihatarishi; na

(vii) Kutoa mwongozo na ushauri ili kuhakikisha kuwa vihatarishi vinatambuliwa, tathminiwa na kupunguzwa.

Divisheni hii itaongozwa na Mkurugenzi na itajumuisha Sehemu mbili (2) zifuatazo: -

(i) Sehemu ya mipango na bajeti; na

(ii) Sehemu ya ufuatiliaji na tathmini.

Sehemu ya mipango na bajeti.

Sehemu hii itakuwa na majukumu yafuatayo:

(i) Kuratibu uandaaji wa mpango kazi wa mwaka, kati na mpango mkakati;

(ii) Kuainisha miradi ,programu,mipango kazi na kuendeleza mikakati ya ukusanyaji wa rasilimali;

(iii) Kushirikiana na wizara ya Katiba na Sheria ,Wizara ya fedha na Uchumi katika uandaaji wa mpango mkakati na bajeti;

(iv) Kutoa msaada wa kiufundi katika mchakato wa kuandaa mpango mkakati na bajeti; na

(v) Kuandaa maandiko na makubaliano ya miradi na programu kwa ajili ya kupata rasilimali fedha za ndani na nje ya nchi;

Sehemu hii itaongozwa na Mkurugenzi Msaidizi

Sehemu ya ufuatiliaji na tathimini

Sehemu hii itakuwa na majukumu yafuatayo:

(i) Kufatilia utekelezaji mpango kazi wa mwaka na mpango mkakati;

(ii) Kuandaa ripoti za utekelezaji;

(iii) Kuandaa ripoti ya uendeshaji mashtaka nchini;

(iv) Kutoa michango katika maandalizi ya mipango ya kitaifa ,programu na masuala ya kibajeti ikiwemo uanishaji wa malengo na viashiria vya utendaji;

(v) Kutoa misaada ya kiufundi katika kusimika mifumo ya tathimini na ufuatiliaji;

(vi) Kufanya utafiti na tathmini juu ya matokeo za mipango,miradi na programu;

(vii) Kukusanya maoni ya wadau kuhusiana na huduma zinazotolewa;

(viii) Kuratibu utekelezaji wa mwaka na nusu mwaka;

(ix) Kuandaa , kutekeleza na kuhuisha mpango wa usimamizi wa vihatarishi;

(x) Kuandaa na kusimamia rejesta ya vihatarishi; na

(xi) Kutoa mwongozo na ushauri ili kuhakikisha kuwa vihatarishi vinatambuliwa, tathminiwa na kupunguzwa.

Sehemu hii itaongozwa na Mkurugenzi Msaidizi