Divisheni ya Makosa ya Udanganyifu, Utakatishaji Fedha na Rushwa
Divisheni ya Makosa ya Udanganyifu, Utakatishaji Fedha na Rushwa
Lengo: kutoa utaalamu na huduma ya mashtaka kwa makosa ya udanganyifu, utakatishaji fedha, rushwa, mazingira na mali asili.
Majukumu
Divisheni hii itakuwa na majukumu yafuatayo:
- (i)Kupitia na kutoa ushauri kwenye sera. Sheria, kanuni , miongozo na viwango katika usimamizi wa makosa ya udanganyifu , utakatishaji fedhana rushwa;
- (ii)Kuratibu kesi za rushwa katika mahakama kuu kitengo cha makosa ya rushwa na uhujumu uchumi na mahakama za chini;
- (iii)Kuratibu taasisi zinazotekeleza sheria katikamakosa ya udanganyifu,utakatishaji fedha,rushwa na masuala yanayohusiana nayo;
- (iv)Kusimamia ufunguaji na uendeshaji wa kesi za udanganyifu na rushwa katika ngazi za mikoa na wilaya;
- (v)Kufungua na kuendesha kesi za rushwa na udanganyifu;
- (vi)Kusimamia mapitio ya majalada ya kesi za utakatishaji fedha, rushwa na udanganyifu;
- (vii)Kuratibu ushirikiano na mashirika ya kitaifa, kimataifa na kikanda pamoja nawadau katika kupambana na makosa ya udanganyifu , utakatishaji fedha na rushwa;
- (viii)Kusimamia kesi za rufaa na maombi yanayohusiana na makosa ya udanganyifu, utakatishaji fedha na rushwa; na
- (ix)Kushughulikia kesi za rufaa na maombi yanayohusiana na rushwa na udanganyifu.
- Divisheni hii itaongozwa na Mkurugenzi na itakuwa na sehemu (3) kama ifuatavyo:
- (i)Sehemu ya makosa ya udanganyifu na utakatishaji fedha;
- (ii)Sehemu ya makosa ya rushwa; na
- (iii)Sehemu ya mazingira na mali asili.
- Sehemu ya makosa ya udanganyifu na utakatishaji fedha
- Sehemu hii itakuwa na majukumu yafuatayo:
- (i)Kutathmini na kushauri kuhusiana na ufanisi wa Sera, Sheria, Kanuni, Miongozo na viwango katika usimamizi wa kesi za udanganyifu na utakatishaji fedha na kupendekeza maboresho;
- (ii)Kuwasiliana na taasisi zinazotekeleza sheria katika masuala yanayohusiana na makosa ya udanganyifu na utakatishaji fedha na yanayohusiana nayo;
- (iii)Kufuatilia ufunguaji na uendeshaji wa kesi za makosa ya udanganyifu na utakatishaji fedha katika ngazi za mikoa na wilaya;
- (iv)Kufungua na kuendesha kesi zinazohusiana na makosa ya rushwa na udanganyifu;
- (v)Kusimamia na kushauri uendeshaji wa kesi za makosa ya udanganyifu na utakatishaji fedha ili kuleta tija;
- (vi)Kufanya mapitio ya majalada kutoka vyombo chunguzi na kutoa maelekezo stahiki kuhusiana na makosaya udanganyifu na utakatishaji fedha;
- (vii)Kuratibu ushirikiano na mashirika ya kitaifa , kimataifa na kikanda pamoja na wadau katika mapambano dhidi ya makosa ya udanganyifu na utakatishaji fedha; na
- (viii)Kushughulikia kesi za rufaa na maombi yanayohusiana na makosaya udanganyifu na utakatishaji fedha.
- Sehemu hii itaongozwa na Mkurugenzi Msaidizi.
- Sehemu ya Makosa ya Rushwa
- Sehemu hii itakuwa na majukumu yafuatayo:
- (i)Kutathmini na kushauri kuhusiana na ufanisi wa Sera, Sheria, Kanuni,Miongozo na viwango katika usimamizi wa kesi za rushwa na kupendekeza maboresho;
- (ii)Kuwasiliana na taasisi zinazotekeleza sheria za makosa ya rushwa na yanayohusiana nayo;
- (iii)Kusimamia ufunguaji na uendeshaji wa kesi za rushwa na yanayohusiana nayo katika ngazi ya mkoa na wilaya;
- (iv)Kufungua na kuendesha kesi za rushwa na masuala yanayohusiana nayo;
- (v)Kusimamia na kushauri njia bora za uendeshaji wa kesi za rushwa;
- (vi)Kufanya mapitio ya majalada kutoka vyombo chunguzi na kutoa maelekezo stahiki kuhusiana makosa ya rushwa;
- (vii)Kuratibu ushirikiano na mashirika ya kitaifa, kimataifa na kikanda pamoja na wadau katika mapambano dhidi ya rushwa; na
- (viii)Kushughulikia rufaa na maombi ya kesi za rushwa.
- Sehemuhii itaongozwa na Mkurugenzi Msaidizi.
- Sehemu ya Makosa ya Mazingira na Maliasili
- Sehemu hii itakuwa na majukumu yafuatayo:
- (i)Kutathmini na kushauri kuhusiana na ufanisi wa Sera, Sheria, Kanuni,Miongozo na viwango katika usimamizi wa kesi za mazingira na mali asili na kupendekeza maboresho;
- (ii)Kuwasiliana na taasisi zinazotekeleza sheria za makosa ya mazingira na mali asili;
- (iii)Kusimamia ufunguaji na uendeshaji wa kesi za mali asili na mazingira;
- (iv)Kusimamia na kufuatilia kesi za mazingira na mali asili zinazoendeshwa na taasisi nyingine;
- (v)Kusimamiamapitio ya majalada ya kesi za mazingira na mali asili kutoka vyombo chunguzi;
- (vi)Kuratibu ushirikiano na mashirika yakimataifa na kikanda pamoja na wadau katika mapambano dhidi ya makosa ya mazingira na mali asili; na
- (vii)Kushughulikia rufaa na maombi ya kesi za mali asili na mazingira.
- Sehemu hii itaongozwa na Mkurugenzi Msaidizi.